歌词
Sikomi -Diamond Platnumz
Written by:Nasibu Abdul Juma Issaack
Wanasemaga mapenzi safari
Unavyopita ndo jinsi unajongea
Ila niendako ni mbali sijui ka ntafika sababu natembea
Niliposikiaga habari
Yakisifika nikakesha nangojea
Akabariki jalali na nikawika muziki nikauotea
Ile pruuu mpaka macca
Nikadandiaga bongo movie
Kumbe mapenzi hayataki haraka
Ni kama tango natia tu chumyi
Mwenzenu nikaoza haswa
Na kujitia kitandani mjuzi
Eti nataka fukuza paka
Badala ya mbwa nikafuga mbuzi
Hhhmmm
Wivu ukanifanya nikagombana na marafiki
Ugomvi na mamangu akiniambia siambiliki
Moyo ukanambia nasibu sasa mapenzi basi
Ila nang'ang'ania najaribu kuipinga nafsi
Esma ananiambia mdogo wangu mapenzi basi
Ila nang'ang'ania
Nikiumizwa na huyu kesho nna mwingine
Ooh mbona sikomi
Sikomiii
Sikomi
Licha ya mateso haya
Najiuliza oh sikomiii
Oh sikomi mbona sikomiii
Mbona jamani
Sikomi
Licha ya mateso haya
Hhhhmmm
Aliyonifanyia wa central
Haki ya mungu siyawezi sema
Ila nimejifunza kesho nisiwaamini wacheza sinema
Moyo walinipatia mateso
Siwezi kumeza siwezi tema
Ndio maana sikushanga ile ghafla
Toka ccm kwenda chadema
Wanasema kitanda ukitandika sharti ukilalie
Nikajitia ukamanda yatakwisha
Wacha nivumilie
Kila kiza kikitanda
Ndo visa machozi me nilie
Penzi yakatia parapanda
Kuwaita waje washambulie
Aah
Acha na penny we darling
Nilio muhongaga gari aliponambia ana mimba
Mwisho wa siku akaichomoa chaliiiii
Mola akanitunuku zari
Akanzalia dume na mwali
Niliyvo mjinga nikacheat aibu mpaka
Kwa vyombo vya habari
Moyo unanambia nasibu sasa mapenzi basi
Ila nang'ang'ania najaribu kuipinga nafsi
Lizer ananiambia simba mapenzi basi
Ila nang'ang'ania
Nikiumizwa na huyu kesho nna mwingine
Ooh mbona sikomi mboooona
Sikomiii mbona jamani
Sikomi
Licha ya mateso haya
Eh nishafumania oh sikomiii
Nikafumaniwa mimi sikomi
Nishagombana na watu sikomiii
Licha ya mateso haya
Licha ya mateso haya
专辑信息
1.Sikomi